WANAFUNZI WA MARA SEKONDARI WAANDAMANA WAKIDAI MATIBABU BORA NA CHAKULA BORA

WANAFUNZI WA MARA SEKONDARI WAKIWA KATIKA MAANDAMANO             










Wanafunzi wa shule ya  Sekondari  ya Mara iliyopo  Manispaa ya Musoma mkoani Mara leo wameandamana kuelekea ofisi za mkoa  kile wanachodai kuwa katika shule hiyo hakuna utaratibu  bora wa matibabu na kubadilishiwa  ratiba ya Chakula.

Wakiongea mbele ya Afisa Elimu Mkoa wa Mara Bw Hamis Lisu katika viwanja vya Posta Manispaa ya Musoma, Baadhi ya wanafunzi hao wamesema kuwa kubadilika kwa ratiba ya chakula na kutokuwepo kwa huduma bora za matibabu ndio hali iliyopelekea wao kuandamana ili kufikisha kilio chao katika ngazi ya mkoa.

Wamesema kuwa walipokuwa kidato cha tano ratiba ya kula wali,nyama pamoja na mboga za Majani ilikuwa ni mara mbili kwa wiki lakini tangu January Mwaka huu walielezwa kubadilika kwa ratiba ya chakula kutokana na kugoma kwa mzabuni na hivyo kula wali na nyama mara moja kw wiki  huku mboga za majani hazipatikani kabisa kama wanavyobainisha Alex Mirumbe pamoja na Emmanuel William.

Akiongea mara baada ya kuwasikiliza wanafunzi hao,Afisa elimu Mkoa wa Mara Bw Hamis Lisu aliwaahidi wananfunzi hao kukutana na uongozi wa wilaya na kisha kwenda shuleni hapo ili kutatua madai ya wanafunzi hao.


Mwisho


Comments

Popular posts from this blog

KATI YA KUKU NA YAI KIPI KILITANGULIA?

NGUO ZA NDANI ZINAZOBANA KWA WANAUME ZINAATHIRI UWEZO WA MBEGU ZA KIUME KUWEZA KUTUNGA MIMBA

TOZI GAMBA AFUNIKA SHOW YAKE NA THE TRACK MASTERS DJS BWALO LA POLISI MWISENGE SIKU YA CHRISTMAS