WATAKAO FELI MTIHANI WA KIDATO CHA PILI KURUDIA DARASA

Wanafunzi
Wakati wanafunzi wa kidato cha pili wakitarajia kufanya mtihani wa taifa wiki ijayo, Serikali imesema watakao feli watarudia darasa hilo.



Kauli hiyo imetolewa na katibu mkuu wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi profesa Sifuni Mchome alipokua akizungumza na waandishi wa habari jijini dar es salaam. Alisema jumla ya wanafunzi 531, 457 wa kidato cha pili wanatarajia kufanya mtihani huo nchi nzima.

“ watakao feli watarudia darasa hilo na watakao feli mara ya pili serikali itaangalia uwezekano wa kuwapeleka shule za ufundi au kuendelea na shule kama wanafunzi wa kujitegemea” alisema Profesa sifuni.
Alisema mtihani huo utaanza October 7 hadi 21 mwaka huu katika vituo takribani 4,437 vilivyosajiliwa kwa ajili ya kufanyia mitihani nchi nzima na wanafunzi waliojiandikisha kufanya mitihani hiyo wasichana ni 270,734 sawa na asilimia 50.1 na wavulana ni 260,723 sawa na asilimia 49.1 ambao ni sawa na ongezeko la asilimia 3.1 ikilinganishwa na watahiniwa wa mwaka jana ambao walikua 4,297.

Aidha alisema kwa upande wa makundi maalum yenye mahitaji maalumu wenye uoni hafifu ni 89 na wasiona ni 93.

Comments

Popular posts from this blog

KATI YA KUKU NA YAI KIPI KILITANGULIA?

NGUO ZA NDANI ZINAZOBANA KWA WANAUME ZINAATHIRI UWEZO WA MBEGU ZA KIUME KUWEZA KUTUNGA MIMBA

TOZI GAMBA AFUNIKA SHOW YAKE NA THE TRACK MASTERS DJS BWALO LA POLISI MWISENGE SIKU YA CHRISTMAS