RAIS MUGABE ATIMIZA MIAKA 89 ASEMA JUKUMU LA KUIONGOZA NI AMRI YA MWENYEZI MUNGU

MUGABE
Wafuasi wa Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe wamekusanyika katika mji wa Bindura wenye migodi ili kusherehekea rasmi Bwana Mugabe kutimiza miaka 89.
Ripoti zinasema sherehe hiyo inagharimu dola 600,000 kutokana na mchango wa makampuni.
Wenye maduka mjini Bindura wanasema waliamrishwa kufunga maduka mapema hapo jana, ili kusaidia kusafisha mji kwa ajili ya party ya siku ya kuzaliwa ya Bwana Mugabe.

Hii ni sherehe ya pili ya Bwana Mugabe kutimiza miaka 89.
Katika party ya kwanza iliyofanywa mwezi uliopita Bwana Mugabe alisema jukumu lake la kuongoza Zimbabwe amepewa na Mungu - ni amri ya Mwenyezi Mungu.

Wapinzani wake wana wasi-wasi kuwa wafuasi wa Bwana Mugabe wanapanga kuanza tena ghasia na vitisho wakati nchi inajitayarisha kwa uchaguzi mkuu utaofanywa mwaka huu.
Wanasema tayari ofisi za makundi yanayochunguza uchaguzi zimeshambuliwa na polisi wamenyang'anya watu mamia ya redio za kuweza kusikiliza matangazo ya mbali.

Zimbabwe itafanya kura ya maoni kuhusu katiba mpya katika majuma mawili yajayo.Chanzo bbc swahili


Comments

Popular posts from this blog

KATI YA KUKU NA YAI KIPI KILITANGULIA?

NGUO ZA NDANI ZINAZOBANA KWA WANAUME ZINAATHIRI UWEZO WA MBEGU ZA KIUME KUWEZA KUTUNGA MIMBA

MADHARA YA KUTUMIA DAWA ZA SILKONI KUONGEZA MAKALIO KWA WANAWAKE