MISS MARA 2013 SASA KUFANYIKA MWANZONI MWA MWEZI WA SITA

Mkurugenzi wa Homeland Entertainments & Promotion Bwana Godsos Mkama( Kulia) Akisisitiza kuwa Mwaka Huu lazima Mkoa wa Mara Utachukua Taji la Miss Tanzania Bila Ubishi.






Mkurugenzi wa kampuni ya Homeland Entertainments & Promotions ya Mjimi Musoma Bwana Godsos Mkama amesema shindano la Miss Mara kwa mwaka huu litafanyika wiki ya kwanza ya mwezi wa sita.

Akiongea na Chibasa Media House amesema kwa mwaka huu shindano hilo litafanyika baada ya kuwapata wawakilishi kutoka wilaya zote za mkoa wa mara ili kuingia kambini rasmi.

Amesema kuwa kwa mwaka huu amejipanga vilivyo kwa udhamini wa kampuni ya bia ya TBL atahakikisha washiriki wake wanafanya vyema kuanzia ngazi ya kanda hadi taifa.

Mkama ameongeza kuwa kwa mwaka huu shindano hilo litapambwa na wasanii wakali wa mziki wa kizazi kipya toka dar es salaam na musoma na wasanii hao wako kwenye hatua za mwisho za mazungumzo ili wasaini mkataba.

Endelea kutembelea mtandao huu ili uweze kufahamu maandalizi ya shindano hilo la miss mara 2013 na wasanii watakao kuja. 


Comments

Popular posts from this blog

KATI YA KUKU NA YAI KIPI KILITANGULIA?

NGUO ZA NDANI ZINAZOBANA KWA WANAUME ZINAATHIRI UWEZO WA MBEGU ZA KIUME KUWEZA KUTUNGA MIMBA

MADHARA YA KUTUMIA DAWA ZA SILKONI KUONGEZA MAKALIO KWA WANAWAKE