ZANZIBAR HEROES YAFUTWA KWA UTOVU WA NIDHAMU KWA KUGAWANA FEDHA BILA UONGOZI WA CHAMA CHA MPIRA ZANZIBAR

Kikosi cha Timu ya Zanzibar Heroes
Kikosi cha timu ya Zanzibar Heroes kimefutwa kwa
utovun wa nidhamu, baada ya kushika nafasi ya tatu kikosi hicho katika
michuano ya CECAFA, wamegawana fedha bila ya uongozi wa chama cha mpira Zanzibar kufahamu.
Chama cha Soka Zanzibar (ZFA) kimechukua uwamuzi wa kuivunja rasmi timu ya taifa,
Zanzibar Heroes kufuatia kitendo utovu wa nidhamu kilichofanywa na wachezaji wa timu hiyo,kuamuwa kugawana fedha walizopata baada ya kushika
nafasi ya tatu katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki
na Kati, CECAFA Tusker Challenge yaliyomalizika hivi karibuni mjini
Kampala, Uganda.

Timu ya Zanzibar heroes ilizawadiwa kiasi cha dola za Kimarekani
10,000 baada ya kuifunga timu ya taifa ya Bara, Kilimanjaro Stars kwa
penalti 6-5, baada ya kumalizika mchezo kwa sare ya 1-1.

Inadaiwa kuwa wachezaji hao waliamua kugawana fedha hizo kwa madai
kuwa wamekuwa wakidhulumiwa fedha zao kila wanaposhiriki katika
mashindano ya kimataifa, kutokana na kitendo hicho Chama cha Soka
Zanzibar (ZFA), kimewafungia wachezaji 16, kwa muda usiyojulikana
kucheza soka popote duniani.
ZFA.

Katibu Mkuu wa ZFA Taifa, Kassim Haji Salum, akielezea tukio hilo amesema
haijawahi kutokea wachezaji wa timu hiyo kudhulumiwa haki yao,
akikumbushia fedha za zawadi walizopata mwaka 1995 katika mashindano
kama haya yaliyofanyika nchini Uganda na Zanzibar ikafanikiwa kutwaa
ubingwa na mwaka 2009 waliposhika nafasi ya tatu na mara zote walipewa
stahili zao.Chanzo Nifahamishe

 

Comments

Popular posts from this blog

KATI YA KUKU NA YAI KIPI KILITANGULIA?

NGUO ZA NDANI ZINAZOBANA KWA WANAUME ZINAATHIRI UWEZO WA MBEGU ZA KIUME KUWEZA KUTUNGA MIMBA

MADHARA YA KUTUMIA DAWA ZA SILKONI KUONGEZA MAKALIO KWA WANAWAKE