TETESI ZIMEENEA KATIKA MITANDAO YA KIJAMII KUWA MIKE TYSON ADAIWA KUBADILISHA JINSIA

MIKE TYSON

BINGWA wa zamani wa ndondi uzito wa juu, Mike Tyson anadaiwa kubadilisha jinsia kutoka kuwa hali ya kiume na kuwa kike.

Habari za kufanyiwa upasuaji huyo kwenye hospitali moja mjini, Beverley Hills, Marekani ziliteka mitandao kadhaa ya kijamii, huku pia gazeti la The Standard likiwa na habari hiyo.
Hata hivyo, habari hizo hazijathibitishwa ramsi ingawa mpaka jana jioni mitandano mingi ya kijamii ilikuwa na taarifa hizo.

Bingwa huyo wa zamani aliyejitaja kama Ć«Mwanaume mbaya dunianiĆ­, mzaliwa wa Brooklyn, aliwaambia waandishi wa habari kuwa siku kwanza atakayopata hedhi (kuona siku zake) ndiyo itakuwa kamilisho la ndoto yake.

Lakipi pia katika kuhakikisha anakamilisha dhamira yake ya kuwa mwanamke, amesema kuanzia muda huo jina lake ramsi sasa litakuwa Michelle.

Baadhi ya watu wanaweza kudhani mimi ni mtu wa ajabu kwa sababu sasa ni mwanamke," alisema bingwa huyo wa zamani wa ndondi aliyewahu kuhukumiwa kwa shitaka la kubaka.
Upasuaji wa kubadilisha jinsia ya Tyson ulichukua takribani masaa 16, akibadilishwa sura, rangi na mambo mengine ya kumfanya avutie kama mwanamke.

Pamoja na ubabe wangu ulionifanya kuwa mpiganaji mzuri, sikuwahi kupoteza hali yangu ya uanamke na nilijua ipo siku moja matiti yataota na pia nitakuwa na sehemu za siri za mwanamke.
Tyson, maarufu kama 'Iron Mike au Iron Maiden', aliyewahi kumng'ata meno bondia, Evander Holyfield walipodundana mwaka 1996, alipandikizwa homoni za kike zitakazomfanya kuwa na tabia za jinsia hiyo.
Tyson, akiwa amevalia wigi, suruali aina jeans yenye nyeusi na fulana ya rangi ya Bluu na kuonekana mwenye furaha, alisema kubadilishwa kwake viungo na kuwekwa vya kike, kunathibitisha mwisho wa tabia yake mbaya.

Pamoja na watangazaji wa ndondi kushangazwa na hatua hiyo ya Tyson, lakini wengi wamekubali kwamba kuna mabadiliko ya kitabia yameonekana. "Amabadilisha kimavazi, mwonekano na kizuri zaidi amekuwa mpole," taarifa zilidai.

Kwa siku za hivi karibuni kumekuwa na taarifa mbalimbali za uzushi zikiwahusu watu maarufu, ambapo katika ya mwaka huu msanii Eddie Murphie alidaiwa kufa katika ajali ya boti ya kuteleza kwenye barafu.
Msanii mwingine aliyehushishwa na uzushi huo ni Will Smith ambaye naye alikumbwa na kadhia ya kudaia kufa. Wote wako hai mpaka sasa.Chanzo gazeti la Mwananchi

Comments

Popular posts from this blog

KATI YA KUKU NA YAI KIPI KILITANGULIA?

NGUO ZA NDANI ZINAZOBANA KWA WANAUME ZINAATHIRI UWEZO WA MBEGU ZA KIUME KUWEZA KUTUNGA MIMBA

TOZI GAMBA AFUNIKA SHOW YAKE NA THE TRACK MASTERS DJS BWALO LA POLISI MWISENGE SIKU YA CHRISTMAS