TAFITI ZA KISAYANSI ZINAONYESHA KUWA ULAJI SANA WA NYAMA NYEKUNDU UNASABABISHA UPOFU

ULAJI SANA WA NYAMA NEKUNDU UNASABABISHAUPOFU
Watu wanaopenda sana kula nyama nyekundu kama vile nyama za ng'ombe , mbuzi au 'kitimoto' wana uwezekano mkubwa wa kupata upofu kwenye uzee wao.

 Matokeo ya utafiti wa wanasayansi umegundua kwamba watu wanaopenda kula sana zaidi ya mara kumi kwa wiki nyama za ng'ombe, mbuzi au kondoo na nguruwe wana uwezekano wa asilimia 50 wa kupata upofu kulinganisha na wale wanaokula nyama hizo chini ya mara tano kwa wiki.

Utafiti huo pia umeonyesha kuwa watu wanaopenda sana kula nyama za kuku walionekana kuwa na kinga dhidi ya ugonjwa unaosababisha upofu kutokana na kuharibika kwa retina ya jicho unaojulikana kitaalamu kama Age-related macular degeneration (AMD) ambao husababisha upofu kwa wazee wenye umri zaidi ya miaka 50.

Utafiti huo ulifanywa na chuo kikuu cha Melbourne cha nchini Australia ambapo wanaume na wanawake 5,600 wenye umri wa kwenye miaka ya hamsini na sitini walifanyiwa majaribio kwa miaka 13.

Ingawa ulaji wa nyama nyekundu ulionekana una madhara, watu walioonekana kupenda kula sana nyama ya kuku mara tatu hadi nne kwa wiki walionyesha kuwa na uwezekano mdogo sana wa asilimia 57 kupata upofu kulinganisha na wale waliokuwa wakila nyama za kuku mara moja au mbili kwa wiki.

Ugonjwa wa AMD kawaida huanza kushambulia mtu anapofikisha umri wa miaka 50 ambapo macho huanza kuvuja vimiminika ambavyo huharibu uwezo wa kuona.

Ni mtu mmoja tu kati ya kumi wanaokumbwa na ugonjwa wa AMD hufanikiwa kupata tiba.Chanzo Nifahamishe

Comments

Popular posts from this blog

KATI YA KUKU NA YAI KIPI KILITANGULIA?

NGUO ZA NDANI ZINAZOBANA KWA WANAUME ZINAATHIRI UWEZO WA MBEGU ZA KIUME KUWEZA KUTUNGA MIMBA

TOZI GAMBA AFUNIKA SHOW YAKE NA THE TRACK MASTERS DJS BWALO LA POLISI MWISENGE SIKU YA CHRISTMAS