NGARIBA HUKO MUGUMU WILAYANI SERENGETI WAMESEMA WATAACHA SHUGHULI HIYO PINDI WAZAZI WATAKAPO ACHA KUWAPELEKA WATOTO KWAO KWA AJILI YA KUKEKETWA
BAADHI ya wanawake wanaoendesha vitendo vya ukeketaji watoto wa
kike, maarufu kwa jina la Ngariba, wilayani Serengeti, Mara, wamesema
hawawezi kuacha kazi hiyo hadi pale wazazi wenyewe watakapoacha
kuwapelekea watoto wao kwa ajili ya kuwakeketa.
Akiwawakilisha wenzake juzi, mmoja wa mangariba hao, Agnes Thomas, ambaye ameshiriki kikao cha kupiga vita ukeketaji, kilichoandaliwa na shirika lisilokuwa la kiserikali la Mara Inter African Commitee, alisema ni vigumu kuacha kazi hiyo, kwani bado wazazi wengi, wana mwamko wa kuwapelekea watoto wao, ili wakeketwe kwa lengo la kutimiza mila zao.
Agnes alisema pamoja na kazi hiyo kuwapatia kipato, lakini ngariba wanaweza kuiacha pale tu wazazi na walezi, watakapobadilika na kuacha tabia ya kuwapelekea watoto.
Aidha, wazee wa kimila walioshiriki kwenye kikao hicho, walishauri ili kukomesha ukeketaji; elimu inapaswa kutolewa, ili jamii ifahamu madhara yake.
Aidha, katika kikao hicho wazee wa kimila pia walipendekeza itafutwe njia mbadala ya kukeketa watoto wa kike, ili waweze kutimiza mila zao.
Moja ya njia waliyopendekeza ni kimwingiza msichana katika chumba kinachotumika kukeketea na kisha kuwamwagia unga na kumpaka usoni bila ya kumkeketa.Chanzo Ahmed Makongo
Akiwawakilisha wenzake juzi, mmoja wa mangariba hao, Agnes Thomas, ambaye ameshiriki kikao cha kupiga vita ukeketaji, kilichoandaliwa na shirika lisilokuwa la kiserikali la Mara Inter African Commitee, alisema ni vigumu kuacha kazi hiyo, kwani bado wazazi wengi, wana mwamko wa kuwapelekea watoto wao, ili wakeketwe kwa lengo la kutimiza mila zao.
Agnes alisema pamoja na kazi hiyo kuwapatia kipato, lakini ngariba wanaweza kuiacha pale tu wazazi na walezi, watakapobadilika na kuacha tabia ya kuwapelekea watoto.
Aidha, wazee wa kimila walioshiriki kwenye kikao hicho, walishauri ili kukomesha ukeketaji; elimu inapaswa kutolewa, ili jamii ifahamu madhara yake.
Aidha, katika kikao hicho wazee wa kimila pia walipendekeza itafutwe njia mbadala ya kukeketa watoto wa kike, ili waweze kutimiza mila zao.
Moja ya njia waliyopendekeza ni kimwingiza msichana katika chumba kinachotumika kukeketea na kisha kuwamwagia unga na kumpaka usoni bila ya kumkeketa.Chanzo Ahmed Makongo
Comments
Post a Comment