MAMA ATAKA KUJIUA KWA KUNYWA SUMU BAADA YA KUFIWA WATOTO WATATU
Mama
mmoja Mkoani Mara, amechukuwa uwamuzi wa kunywa sumu baada ya kugunduwa
watoto wake watatu wamefariki dunia, watoto hao walikufa kwa kukosa
hewa, baada ya kuacha jiko la mkaa lililokuwa limeinjikwa maharage
likiwa linawaka na kwenda kulala.
Mama
huyo alichukua uwamuzi huo mgumu na wahatari wa kunywa sumu baada ya
kuamka na kugunduwa kuwa watoto wake watatu wamefariki dunia, mama huyo
aliwaishwa hospitali na kufanikiwa kutapishwa sumu aliyokunywa. Watoto hao walikufa kutokana na kukosa hewa katika chumba walichokuwa wamelala ambacho kulikuwa na jiko la mkaa lililokuwa likipika maharage, lna kusababisha kukosa hewa na kupelekea vifo kwa watoto hao. Watoto hao watatu waliyofariki ni wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Nyangoto, iliyopo katika Tarafa ya Ingwe wilayani Tarime Mkoani Mara, Naomi Nyasenso darasa la saba, Magreth Nyasenso darasa la nne na Debora Nyasenso darasa la kwanza. Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Tarime, Kamishina Msaidizi Justus Kamugisha, amewashauri wananchi kujenga nyumba na kuweka madirisha makubwa, kwani nyumba hiyo ingekuwa na madirisha makubwa ya kuingiza hewa, ajali hiyo isingetokea.Chanzo Nifahamishe |
||
Comments
Post a Comment