KIPIMO CHA X-RAY KATIKA HOSPITALI YA MKOA WA MARA KIMEFANYIWA MATENGENEZO

MGANGA MFAWIDHI WA HOSPITALI YA MKOA WA MARA IRAGI NGERAGEZA AKITOA MAELEZO KWA BAADHI YA WAANDISHI WA HABARI.

BAADHI YA WAANDHI WA HABARI MKOANI MARA WAKIWA NA MGANGA MFAWIDI WA HOSPITALI YA MKOA WA MARA KUTOKA KUSHOTO NI HELLEN MAGABE, IRAGI NGERAGEZA AMBAYE NDIE MGANGA MFAWIDHI, EMMANUEL CHIBASA NA LAZARO KAAJI


Baadhi ya wagonjwa wanaokwenda hospitali ya Mkoa wa Mara kupima kipimo cha X-ray wamelalamikia uongozi wa hospitali hiyo kutotoa taarifa kwa wagonjwa baada ya kukosekana kwa huduma hiyo kwa muda.

Wakiongea na gazeti hili leo wakiwa nje ya chumba cha x-ray mmoja wa wagonjwa Bi Mage Hilary amesema toka siku ya jumatatu amekuwa akiwahi kila siku asubuhi ili kupata huduma hiyo lakini ameshindwa kuipata na hakuna taarifa yoyote toka kwa daktari kwa nini hataki kuwahudumia.

“Ndugu mwandishi hii sio haki kabisa we fikiria toka asubuhi tuko hapa na hakuna taarifa yoyote toka kwa daktari kwanini huduma haitolewi tunawaona tu madaktari wanapita hapa wanatuona kama majengo je hii ni haki kweli” alisema bi Mage.

Naye Piter Majaliwa mkazi wa kigera manispaa ya musoma amesema kuwa kwa muda wa wiki moja amekuwa akifika hospitalini hapo kupata huduma hiyo baada ya kupata ajali ya pikipiki na kuumia ubavu wa kushoto lakini kila anapofika hapati huduma na hivyo anashindwa kuelewa tatizo ni nini kwani hakuna taarifa iliyotolewa kwao ili wajue nini cha kufanya.

Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa huduma ya x-ray katika hospitali hiyo ilikuwa haipatikani kwa muda wa wiki mbili kutokana na mashine kuharibika ghafla.
Mganga mfawidhi wa hospitali hiyo Iragi Ngerageza amesema kuwa mashine ya x-ray iliharibika ghafla wiki mbili zilizopita na walikuwa wanawasubiri mafundi kutoka kampuni ya Philips ambayo ndio walipewa tenda ya kufunga na kutengeneza mashine hiyo.

Amesema baada ya tatizo hilo kutokea walishindwa kuchukua mafundi sehemu nyingine kwa ajili ya kuitengeneza kwani tayari walishaweka makubaliano na kampuni ya Philips kuwa wao ndio watakua wanaifanyia matengenezo mashine hiyo, na kilichosababisha mashine hiyo kuharibika ni kutofanyiwa matengenezo kwa muda mrefu.

Ameongeza kuwa uongozi wa hospitali hiyo umejitahidi kulishughulikia tatizo hilo na tayari wamefanikiwa kurejesha huduma hiyo lakini changamoto inayowabili pia ni uchache wa madakitari na wauguzi katika kutoa hudumia.

Aidha amesema kuwa changamoto nyingine inayowakabili ni fedha ambapo ili hospitali iweze kuendesha shuguli zake kwa ufasaha inahitaji shilingi milioni ishirini na sita(26) kwa mwezi lakini wamekuwa wakishindwa kufikia lengo hilo kutokana na sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na swala la rushwa lakini kwa sasa wanatarajia kufikisha lengo la kukusanya kiasi hicho cha pesa ama zaidi baada ya kufanya kazi na watu kutoka taasisi ya kupambana na kuzuia rushwa takukuru.

Comments

Popular posts from this blog

KATI YA KUKU NA YAI KIPI KILITANGULIA?

NGUO ZA NDANI ZINAZOBANA KWA WANAUME ZINAATHIRI UWEZO WA MBEGU ZA KIUME KUWEZA KUTUNGA MIMBA

MADHARA YA KUTUMIA DAWA ZA SILKONI KUONGEZA MAKALIO KWA WANAWAKE