JESHI LA POLISI MARA LAKANUSHA UVUMI WA WATU KUUWAWA KWA KUCHINJWA
JAPHET LUSINGU-KAIMU KAMANDA WA POLISI MARA, MUSOMA |
Jeshi la
Polisi Mkoani Mara limekanusha uvumi wa kutishia wananchi toka kwa baadhi ya
watu wenye nia mbaya kuwa ndani ya mwezi mmoja watu 15 wameuwawa kwa kuchinjwa.
Kwa mujibu
wa taarifa iliyotolewa kaimu kamanda wa Jeshi la Polisi Mara, Musoma Japhet
Lusingu imedai kwamba hivi karibuni kumekua na uvumi kuwa katika Mkoa wa Mara
wananchi wamekuwa wakichinjwa na tayari watu 15 wameuwawa kwa kuchinjwa kitu
ambacho ni uongo.
Kaimu
kamanda huyo amesema kutokana na uvumi huo wamekua wakipokea simu toka kwa
wananchi na viongozi ndani ya manspaa ya Musoma katika kata ya nyakato kwamba
kuna kuna mwanafunzi ameonekana ameuwawa kwa kukatwa kichwa katika makaburi ya
Musoma bus na jeshi la polisi likifuatilia wanakuta ni taarifa za uongo na za
kuwatisha wananchi.
Amesema kuna
matukio mawili wanawake kuuwawa vichakani katika vijiji vya Mmahare kata ya
Etaro ambapo Blandina Peru (28) aliuwawa 2.12.2012 kwa kukatwa koromeo na
kubakwa na wauaji kabla ya kumuua wakati akiwa porini akikata kuni na watuhumiwa
wa tukio hilo bado hawajakamatwa.
Tukio la
pili lilitokea Kabegi kata ya Nyakatende wilayani butiama ambapo Sabina Mkireri
(44) mkazi wa kijiji cha kiemba aliwawa kwa kuchinjwa shingo na kichwa chake
kuchukuliwa na watu wasiojulikana katika kijiji cha kabegi na watu sita wanashikiliwa
na jeshi la polisi kwa mahojiano.
Kutokana na
uvumi huo amewatoa hofu wananchi juu ya
mauaji hayo na kuwatahadharisha akina mama hasa maeneo ya vijijini wanapokua
katika shughuli zao za kilimo na utafutaji wa kuni wawe waangalifu na watoe
taarifa mapema wanaposhuku jambo lolote lisilo lakawaida.
Ameongeza
kuwa kwa sasa wanaendelea na msako maeneo mbalimbali ya manispaa ya Musoma na
wilaya ya butiama ambapo kuna watu watano wanashikiliwa na jeshi hilo kwa kwa
makosa yakupatikana na pombe haramu ya gongo na wengine wanashikiliwa kwa
kupatikana na bangi na wote watafikishwa mahakamani baada ya upelelezi
kukamilika.
Katika hatua
nyingine amewataka wananchi wenye taarifa za uhalifu na wahalifu wasisite
kulijulisha jeshi la polisi kupitia kwa viongozi wa maeneo yao.
Comments
Post a Comment