HOSPITALI YA MKOA WA MARA INAKABILIWA NA UPUNGUFU WA BAADHI YA DAWA

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Mara Iragi Ngerageza
Hospitali ya Mkoa wa Mara inakabiliwa na upungufu wa baadhi ya dawa zinazotolewa na bohari ya dawa (msd) hali inayopelekea dawa zinazokosekana kununuliwa kwenye maduka binafsi yaliyoteuliwa na serikali.

Akiongea na chibasa blogspot mganga mfawidhi w badoa hospitali hiyo Iragi Ngerageza amesema kuwa bohari ya dawa imekuwa ikiwapa dawa ambazo hazitoshelezi mahitaji ya hospitali hiyo.

Amesema kuwa hivi karibuni hospitali hiyo imenunua dawa kwenye bohari ya dawa zenye thamani ya shilingi 41,190,100 lakini bado kuna mahitaji ya baadhi ya dawa hali inayosababisha wananchi kwenda kununua madawa kwenye maduka ya mitaani.

Katika kukabiliana na tatizo hilo tayari uongozi wa hospitali kupitia kamati yake inafanya jitahada ya kununua dawa ambazo hawakuzipata kutoka bohari ya dawa (msd) kwenda kununua dawa hizo kwenye maduka ya watu binafsi ambayo yameteuliwa na serikali.

“Wananchi wanatakiwa kuelewa kuwa tunaupungufu wa baadhi ya dawa lakini tunafanya jitahada za kununua dawa hizo ili kuwawezesha wananchi kupata dawa hizo” alisema


Ili kukabiliana na changamoto hiyo ameiomba serikali kuiwezesha bohari ya dawa kutoa dawa kulingana na mahitaji husika ili kuboresha huduma ya afya kwa jamii hususani wale wanaokwenda kutibiwa katika hospitali hiyo.

Comments

Popular posts from this blog

KATI YA KUKU NA YAI KIPI KILITANGULIA?

NGUO ZA NDANI ZINAZOBANA KWA WANAUME ZINAATHIRI UWEZO WA MBEGU ZA KIUME KUWEZA KUTUNGA MIMBA

MADHARA YA KUTUMIA DAWA ZA SILKONI KUONGEZA MAKALIO KWA WANAWAKE