HAUKIMIWA KWENDA JELA MIAKA SABA KWA KOSA LA KUPATIKANA NA NOTI BANDIA

PESA ZA TANZANIA


MAHAKAMA ya wilaya ya Musoma mkoani Mara, imemhukumu kwenda jela miaka 7 mfanyabiashara  Mayai Justine(28) mkazi wa Nyakato Mshikamano kwa kosa la kupatikana na noti bandia.

Akisoma hukumu hiyo  siku ya ijumaa ,mahakamani hapo  , Hakimu mfawidhi mwandamizi wilaya ya Musoma, Richard Maganga baada ya kuridhika na ushahidi  alimhukumu Justine  kutumikia kifungo cha miaka 7.

Mbele ya hakimu, Mwendesha mashtaka wa serikali  Jonas Kaijage amedai kuwa Bw. Mayai Justine ambaye ni mkazi wa Nyakato Mshikamano mjini Musoma  alipatikana na noti bandia za shilingi elfu 50 April 13 mwaka huu na kufikishwa mahakamani Mei 17, 2012.

akitoa hukumu hiyo Hakimu Maganga amesema kupatikana na noti bandia ni kosa la jinai hivyo ametoa hukumu hiyo hili iwe fundisho kwa wafanyabiashara wanaoweza kufanya kosa kama hilo.


Comments

Popular posts from this blog

KATI YA KUKU NA YAI KIPI KILITANGULIA?

NGUO ZA NDANI ZINAZOBANA KWA WANAUME ZINAATHIRI UWEZO WA MBEGU ZA KIUME KUWEZA KUTUNGA MIMBA

MADHARA YA KUTUMIA DAWA ZA SILKONI KUONGEZA MAKALIO KWA WANAWAKE