CHAMA CHA WAANDISHI WA HABARI WANAWAKE TANZANIA TAMWA KIMETOA MAFUNZO KWA WAANDISHI WA HABARI MKOANI MARA KUANDIKA NA HABARI ZA UKATILI WA KIJINSIA KWA WANAWAKE NA WATOTO

Mkurugenzi wa Chama Cha waandishi wa habari wanawake( TAMWA) Bi Valerie Msoka
Nikielekea Ukumbini kwa ajili ya kuanza mafunzo rasmi GoldLand Hotel
Niko na Dj Cares one kwenye samaaaaaki samaki
Mimi na Rejina toka Sachita Fm Tarime
Eneo la Bustani Goldland Hotel
Baada ya mafunzo kilichofuata nia kupiga picha katika madhali ya GoldLand hotel Tarime
Waandishi wa habari wakisikiliza kwa makini katika mafunzo wa ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto mkoani Mara
Baadhi ya waandishi wa habari mkoani Mara wakiwa katika picha ya pamoja na mkuu wa wilaya ya Tarime John Enjewele, Mkurugenzi mtendaji wa TAMWA Bi Valerie Msoka,Monica Luwando pamoja na Mkurugenzi wa Sachita Fm Peter Mwera





Waandishi wa habari mkoani Mara wamekishukuru Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake(TAMWA) Kwa kuandaa mafunzo ya ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto kwa waandishi wa habari Mkoani Mara.

Wakitoa shukrani zao kwa mkurugenzi mtendaji wa chama cha waandishi wa habari wanawake Bi Valerie Msoka wakati wa kuhitimisha mafunzo ya siku mbili juu ya kuandika na kuripoti habari za ukatili wa kijinsia wamesema kuwa chama hicho kinastahili kupongezwa na kuwa mfano wa kuigwa kwa kutambua mchango wa waandishi wa habari mikoani.

Wamesema kuwa chama hicho ni mfano wa kuigwa na Taasisi na mashirika mengine kwa kuwatumia waandishi wa habari wa eneo husika katika kuandika na kulipoti habari wa ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto mkoani mara na sio kuwatumia waandishi wa habari toka dar es salaam wakati waandishi wa mikoani wapo.

Katika mafunzo hayo ambayo mgeni rasimi alikua mkuu wa wilaya ya Tarime John Enjewele yamewapa mbinu za kuandika habari za ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto.
  
Wamesema  changamoto kubwa inayowakabili  katika kuandika habari za ukatili  fedha kwa ajili ya kusafiri sehemu moja hadi nyingine kwa ajili ya kufanya uchunguzi ili kuandika makala na vipindi vya redio na televisheni.

Kwa mujibu wa tafifiti mbalimbali kuhusu ukatili wa kijinsia kwa wanakwake na watoto mkoa wa Mara ni miongoni mwa mikoa hapa nchini ambayo inafanya vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa asilimia 72 Hivyo wameamua kuandaa mafunzo hayo kwa waandishi ili wasaidie kupunguza vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto kwa waandishi kutoa elimu kwa jamii na kuripoti matukio ya ukatili wa kijinsia kwa wanawake .

Mafunzo hayo yalifanyika wilayani tarime katika ukumbi wa GoldLand hotel kuanzia tarehe 3-4/12/2012.




Comments

Popular posts from this blog

KATI YA KUKU NA YAI KIPI KILITANGULIA?

NGUO ZA NDANI ZINAZOBANA KWA WANAUME ZINAATHIRI UWEZO WA MBEGU ZA KIUME KUWEZA KUTUNGA MIMBA

MADHARA YA KUTUMIA DAWA ZA SILKONI KUONGEZA MAKALIO KWA WANAWAKE