MWANACHUO WA CHUO CHA MUSOMA UTALII ANASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI KWA TUHUMA YA KUMCHOMA VISU MWANACHUO MWENZAKE KISA WIVU WA KIMAPENZI
Mwanachuo wa
chuo cha musoma utalii cha mjini Musoma Rose Kanyambo
(21),ameshambuliwa kwa kisu mgongoni na ubavuni na mwanachuo mwenzake John Ogolla kutokana na wivu wa mapenzi.
Kwa mujibu wa Taarifa toka kwa mganga mfawidhi
wa hospitali ya mkoa wa Mara Irege Ngaregeza, amesema kuwa binti huyo alifikishwa hospitalini hapo
siku ya ijumaa Novemba 2 mwaka huu, ambapo binti huyo alikuwa na jeraha la
kuchomwa kisu mgongoni na ubavuni na alifikishwa hospitalini hapo akiwa na hali mbaya lakini madaktari walijitahidi kuokoa maisha yake na sasa anaendelea
vizuri.
Akizungumza na
waandishi wa habari kwa taabu wodini binti huyo amesema kuwa siku ya ijumaa majira ya saa
mbili asubuhi akiwa chuoni maeneo ya Kamunyonge manispaa ya musoma, Mwanachuo mwenzake anaefahamika kwa jina John Ogolla
alitokea chuoni hapo na kuanza
kumshambulia kwa kumchoma kisu mgongoni mara mbili na ubavuni ambpo hali hiyo ilimpelekea kutokwa na damu nyingi ambapo
alifanikiwa kukimbia hadi alipokuwa anaishi si mbali na chuo lakini kabla hajafika nyumbani alidondoka chini
baada ya kuishiwa nguvu lakini
majirani walifanya jitihada za kumpeleka hospitalini.
Binti huyo
amewambia waandishi wa habari kuwa chanzo cha tukio hilo la kinyama la kuchomwa kisu ni kumkataa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na kijana huyo na mara kwa mara amekuwa akimlazimisha kuwa na uhusiano wa kimapenzi
lakini yeye amekuwa akimkatalia.
Baadhi ya
majirani na wanachuo ambao hawakutaka kutajwa majina yao wamesema kuwa Rose na John wanauhusiano wa kimapenzi kwa muda
mrefu na kijana huyo amekuwa akimsaidia
mambo mengi sana lakini ghafla mpenzi huyo alibadilika na kumkataa bila
sababu za msingi hali iliyopelekea kijana huyo kuchukua maamuzi hayo mazito ya kumchoma kisu.
"kabla yaOgolla kutekeleza tukio hilo alikuwa ameandaa barua ambayo ameandika yenye ujumbe uliosomeka ama kufa
yeye au rose kanyambo na pia alichukua picha ambayo walipiga pamoja na Rose na kuichora
alama ya x kwa kutumia marker pen" alisema shuhuda
Jeshi la
polisi linamshikilia john ogolla kuhusiana na tukio na mara baada ya upelelezi
kukamilika atapandishwa kizimbani.
Comments
Post a Comment