MAMLAKA YA MAPATO MKOA WA MARA YAVUKA LENGO KATIKA UKUSANYAJI KODI TOKA MWEZI JULAI HADI OCTOBA 2012
TANZANIA REVENUE AUTHORIRTY |
Mamlaka ya Mapato ya Mkoa wa Mara imevuka
malengo kwa kukusanya kiasi cha shilingi bilioni 23. na kuvuka lengo lililokusudiwa la shilingi bilioni 22.2 kwa kipindi cha
julai hadi oktoba 2012.
Hayo
yamesemwa leo na meneja wa Mamlaka ya Mapato Mkoa wa Mara Joseph Kalinga
wakati akitoa taarifa ya
ukusanyaji wa mapato kwa mgeni rasmi
katibu tawala wa Mkoa wa Mara Clement Lujaji .
Kalinga
amesema kuwa ili kufanikisha utoaji wa huduma
yenye ubora wa hali ya juu na ya
kuvutia kwa mlipakodi , idara ya huduma na elimu
kwa mlipa kodi ,imekuwa ikitoa
semina mbalimbali zenye lengo la kuwaelimisha
walipa kodi sheria za kodi ,haki
za mlipa kodi,wajibu wa mlipa kodi na wajibu wa mamlaka ya mapato imeongeza
ushirikiano baina ya walipa kodi na watoza
kodi pamoja na kuinua
kiwango cha ulipaji kodi kwa
hiari.
Amesema kuwa hali ya makusanyo kwa mwaka
wa fedha wa 2011/12,Mkoa wa Mara ni sawa na asilimia 86 ya lengo lililowekwa
hapo awali la kukusanya shilingi bilioni 63.5 kwa kuwa mamlaka imefanikiwa
kukusanya shilingi bilioni 54.7
Aidha kalinga ameelezea changamoto zinazowakabili
ni pamoja ongezeko la mahitaji ya mapato
ya serikali katika kutekeleza
mikakati yake ya kupambana na umasikini ,ukwepaji kodi kwa
kupitia njia zisizo rasmi
wakati wa kuingiza bidhaa
nchini au kutoa bidhaa kwenda nje ya
nchi,ukwepaji kodi kwa njia ya kutotoa
risti sambamba na matumizi hafifu ya mashine
za kutolea risti EFD) kwa wasiosajiliwa katika kodi ya
ongezeko la thamani VAT.
Mamlaka kwa
kushirikiana na vyombo vingine vya uthibiti
ambavyo ni jeshi la polisi ,usalama wa taifa na uhamiaji vimeweka
mkakati wa kukabiliana na
changamoto inayohusu ukwepaji kodi
kwa kutumia njia mbalimbali.
Kwa upande
wake mgeni rasmi katibu tawala wa mkoa
wa Mara Clement Lujaji amesema kuwa
dhana ya ulipaji kodi kwa hiari inalenga uelewa wa mlipaji kodi yeye mwenywe na
maendeleo ya taifa na jamii nzima ambapo amesema kuwa kukwepa kodi ni aibu na sio ujasiri ,hivyo amewataka mamlaka ya
mapato kupanua eneo la hamasa kuanzia ngazi ya kata kwa kuwashirikisha madiwani ili kuongeza
walipa kodi, kauli mbiu ulipaji kodi kwa hiari kwa mafanikio ya taifa.
''walipa
kodi ni sisi tukilipa kodi tutaona zahanati zinajengwa ,shule tra panueni
wigo kutolipa kodi ni aibu'' alisema lujaji.
Comments
Post a Comment