KUACHWA KUACHWA KUACHWA NI SHUGULI PEVU

Mwanamke mmoja wa nchini Uingereza ambaye hakuridhishwa na uamuzi wa mpenzi wake kuachana naye, aliamua kumaliza hasira zake kwa kuzamisha meno yake kwenye uume wa mpenzi baada ya kujifanya anaomba msamaha ili uhusiano wao uendelee.


Sinead Walker, mwenye umri wa miaka 40 mkazi wa Bath, Somerset nchini Uingereza alienda kwa mpenzi wake kwaajili ya kuomba msamaha ili mapenzi yao yaendelee kama zamani.

Lakini ghafla mwanamama huyo ambaye ni mama wa mtoto mmoja, alibadili uamuzi wake wa kuomba msamaha na kuamua kumshambulia mpenzi wake Vincent Rennoldson mwenye umri wa miaka 42 kwa kuyabinya kwa nguvu makende yake kabla ya kuamua kuzamisha meno yake ili aukate uume wake.

Mahakama ambayo inasikiliza kesi ya mama huyo kujaribu kuzinyofoa hazina za mpenzi wake, iliambiwa kuwa Sinead akiwa amelewa alienda nyumbani kwa mpenzi wake akisema amekuja kuomba msamaha baada ya kumshambulia Vincent wiki mbili zilizopita baada ya Vincent kuamua kuvunja uhusiano wao.

"Alinisukuma ukutani, aliukamata uume wangu na kuanza kuuvuta kwa nguvu akijaribu kuunyofoa baadae alizamisha meno yake kwenye uume wangu na kuniachia kovu kubwa", alisema Vincent.

Vincent aliongeza kuwa Sinead alikuwa amepiga magoti akijifanya kuomba msamaha kabla ya kuanza shambulio lake hilo.

"Maumivu yake hayaelezeki, nilitokwa na damu nyingi sana, angeweza kuunyofoa kabisa uume wangu", Vincent aliiambia mahakama.

Vincent alielezea kusikitishwa kwake na kitendo hicho ingawa alidai anashukuru mambo hayajaharibika sana na uume wake unafanya kazi kama kawaida.

Sinead atahukumiwa mwezi ujao, ameachiwa kwa dhamana huku akitakiwa asimkaribie mpenzi wake huyo wa zamani

chanzo:Nifahamishe

Comments

Popular posts from this blog

KATI YA KUKU NA YAI KIPI KILITANGULIA?

NGUO ZA NDANI ZINAZOBANA KWA WANAUME ZINAATHIRI UWEZO WA MBEGU ZA KIUME KUWEZA KUTUNGA MIMBA

MADHARA YA KUTUMIA DAWA ZA SILKONI KUONGEZA MAKALIO KWA WANAWAKE