Kamanda wa Polisi Mkoani Mara Asalom Mwakyoma |
Mtu mmoja asiyefahamika majina amekutwa amekufa huku
mwili wake ukiwa na majeraha ya kukatwa na panga katika kijiji cha magunga kata ya buhemba
wilayani butiama mkoani mara
Kamanda wa
polisi wa mkoa wa mara ,kamishina msaidizi Absalom Mwakyoma amethibitisha tukio
hilo ambapo jeshi hilo linafanya uchunguzi ili kubaini marehemu huyo kuwa ni
mkazi wa wapi,ambapo mwili wake umeletwa kuhifadhiwa katika chumba cha maiti
musoma.
Wakati huo
usiku wa kuamkia leo watu wasiofahamika wamevamia nyumba ya kulala wageni ijulikanayo kwa jina la yote heri iliyoko
buhemba wakiwa na silaha aina ya smg huku wakijitambulisha kuwa ni askari
polisi na kuwaamuru wateja wote kufungua
milango na kuwapora simu na fedha na
baada ya kutekeleza wizi huo watu hao walitokomea kusikojulikana.
Jeshi la
polisi mkoani mara linaendelea kuwasaka majambazi hayo ambapo pia limewaomba
wananchi kutoa ushirikiano katika kuwasaka watuhumiwa.
Huko wilayani bunda askari
wa jeshi la polisi na familia zao wilayani Bunda mkoani Mara wameingia katika
adha kubwa ya kulazimika kutumia tochi, vibatari na mishumaa kwa kukosa
umeme takriban mwezi mmoja sasa.
Hatua hiyo imekuja kutokana na taasisi hiyo kushindwa kununua luku za umeme kwa matumizi ya ofisi na katika makazi ya askari hao.
Kwa sharti ya kutotajwa majina baadhi ya askari hao jana wamewaeleza waandishi wa habari waliofika kituoni kujionea hali kuwa umeme unaotumika katika kituo hicho hulipwa na baadhi ya viongozi wa kituo kwa kujitolea.
Walisema katika makazi yao hali ni mbaya zaidi kutokana na serikali kutowapelekea fedha za kununua umeme.
“ tunaishi maisha ya shida sana maana kama kambi ya polisi wanaolinda usalama wa raia tunakosa umeme ni hatari hata kwa usalama wetu” alisema askari mmoja.
Meneja wa Tanesco wilaya ya Bunda Sosthenes Lushamisa alidai kuwa tatizo la polisi kutokuwa na umeme ni lao wenyewe kutokana na kutonunua LUKU katika mita ya TANESCO waliyofungiwa katika kambi yao.
Bw. Lushamisa alifafanua kuwa askari hao wana matumizi makubwa ya umeme lakini wanashindwa kununua umeme wa kutosha na kwa wakati.
Alidai Shirika lake halina tatizo labda la kiufundi jambo ambalo bado hawajapata malalamiko yoyote kutoka polisi.
Kamanda wa polisi mkoa wa Mara Absalum Mwakyoma alipoulizwa kwa njia ya simu na mwandishi wa habari hizi alidai kuwa hana taarifa zozote za polisi Bunda kukosa umeme huku akiahidi kufuatilia.
Wananchi wanaoishi karibu na kambi hiyo wamesikitishwa na kambi la polisi kukaa gizani jambo ambalo ni hatari kwa ulinzi na usalama na kuiomba serikali kuingilia kati suala hilo.
Hatua hiyo imekuja kutokana na taasisi hiyo kushindwa kununua luku za umeme kwa matumizi ya ofisi na katika makazi ya askari hao.
Kwa sharti ya kutotajwa majina baadhi ya askari hao jana wamewaeleza waandishi wa habari waliofika kituoni kujionea hali kuwa umeme unaotumika katika kituo hicho hulipwa na baadhi ya viongozi wa kituo kwa kujitolea.
Walisema katika makazi yao hali ni mbaya zaidi kutokana na serikali kutowapelekea fedha za kununua umeme.
“ tunaishi maisha ya shida sana maana kama kambi ya polisi wanaolinda usalama wa raia tunakosa umeme ni hatari hata kwa usalama wetu” alisema askari mmoja.
Meneja wa Tanesco wilaya ya Bunda Sosthenes Lushamisa alidai kuwa tatizo la polisi kutokuwa na umeme ni lao wenyewe kutokana na kutonunua LUKU katika mita ya TANESCO waliyofungiwa katika kambi yao.
Bw. Lushamisa alifafanua kuwa askari hao wana matumizi makubwa ya umeme lakini wanashindwa kununua umeme wa kutosha na kwa wakati.
Alidai Shirika lake halina tatizo labda la kiufundi jambo ambalo bado hawajapata malalamiko yoyote kutoka polisi.
Kamanda wa polisi mkoa wa Mara Absalum Mwakyoma alipoulizwa kwa njia ya simu na mwandishi wa habari hizi alidai kuwa hana taarifa zozote za polisi Bunda kukosa umeme huku akiahidi kufuatilia.
Wananchi wanaoishi karibu na kambi hiyo wamesikitishwa na kambi la polisi kukaa gizani jambo ambalo ni hatari kwa ulinzi na usalama na kuiomba serikali kuingilia kati suala hilo.
Comments
Post a Comment