CHAMA CHA WANAHABARI WANAWAKE (TAMWA) KUTOA MAFUNZO YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WAANDISHI WA HABARI MKOANI MARA

Chama Cha Wanahabari Wanawake Tanzania

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania(TAMWA) Kinatarajia kuendesha mafunzo kwa Waandishi wa habari Mkoani Mara ili waweze kuibua na kuandika habari za Ukatili wa kijinsia.

Mkurugenzi Mtendaji wa chama hicho Valerie Msoka mafunzo hayo yanalenga kuadhimisha siku 16 za kupinga na kutokomeza ukatili wa kijinsia na lengo kuu la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo waandishi wa Habari  kuripoto swala la ukeketaji na kuandika habari zaidi kuhusu swala hilo.

Tafiti mbalimbali zinaonyesha kuwa Mkoa wa Mara ndio unaongoza kwa vitendo vya ukatili wa kijinsia ukifuatiwa na mkoa wa dodoma.

Waandishi wa habari Mara kupitia chama cha waandishi wa habari mkoa (MRPC) Wanatarajia kushiriki mafunzo hayo kikamilifu ili waweze kuibua na kuripoti habari za ukatili wa kijinsia ili kutokomeza tatizo hilo

Chama hicho hapa nchini kinaendesha miradi kadhaa ikiwa ni pamoja na harakati za usawa wa kijinsia na kuhakikisha kuwa wanawake wanashiriki vyema katika kuchangia maoni ya katiba mpya ili iwe ya demokrasia. 


Comments

Popular posts from this blog

KATI YA KUKU NA YAI KIPI KILITANGULIA?

NGUO ZA NDANI ZINAZOBANA KWA WANAUME ZINAATHIRI UWEZO WA MBEGU ZA KIUME KUWEZA KUTUNGA MIMBA

MADHARA YA KUTUMIA DAWA ZA SILKONI KUONGEZA MAKALIO KWA WANAWAKE