CHAMA CHA WANAHABARI WANAWAKE (TAMWA) KUTOA MAFUNZO YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WAANDISHI WA HABARI MKOANI MARA
Chama Cha Wanahabari Wanawake Tanzania |
Mkurugenzi Mtendaji wa chama hicho Valerie Msoka mafunzo hayo yanalenga kuadhimisha siku 16 za kupinga na kutokomeza ukatili wa kijinsia na lengo kuu la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo waandishi wa Habari kuripoto swala la ukeketaji na kuandika habari zaidi kuhusu swala hilo.
Tafiti mbalimbali zinaonyesha kuwa Mkoa wa Mara ndio unaongoza kwa vitendo vya ukatili wa kijinsia ukifuatiwa na mkoa wa dodoma.
Waandishi wa habari Mara kupitia chama cha waandishi wa habari mkoa (MRPC) Wanatarajia kushiriki mafunzo hayo kikamilifu ili waweze kuibua na kuripoti habari za ukatili wa kijinsia ili kutokomeza tatizo hilo
Chama hicho hapa nchini kinaendesha miradi kadhaa ikiwa ni pamoja na harakati za usawa wa kijinsia na kuhakikisha kuwa wanawake wanashiriki vyema katika kuchangia maoni ya katiba mpya ili iwe ya demokrasia.
Comments
Post a Comment