AUWAWA KIKATILI KWA KUCHOMWA MISHALE NA KUKATWA MAPANGA WILAYANI TARIME AKIGOMBEA ARDHI
Justus Kamugisha Kamanda wa Kanda Maalum ya Kipolisi Tarime na Rorya |
Mtu mmoja
mkazi wa kijiji cha ng’ereng’ere
wilayani tarime ameuwawa kikatili kwa kuchomwa mishale na kukatwa katwa
kwa mapanga .
Akizungumza
na waandishi wa habari kamanda wa kanda maalum ya kipolisi ya Rorya na Tarime
Kamishina Msaidizi Justus Kamugisha
amesema kuwa tukio hilo limetokea jana
majira ya saa mbili asubuhi
ambapo amemtaja aliyeuwawa kwa kuchomwa mishale na mapanga ni Robert Chacha
kabila mkurya -mkira 44)
mkazi wa kijiji cha Ng’ereng’ere Kata ya
Nyamaraga Tarafa ya Inchugu wilayani Tarime.
Kamugisha
amesema kuwa jeshi la polisi linamshikilia juma chacha mwita (22) wa kijiji
cha korotambe ambaye
amekiri kufanya hivyo na wenzake
saba ambao wamekimbia na polisi wanaendelea kuwatafuta.
Chanzo cha
mauaji hayo ni marehemu kulima katika
eneo linalogombaniwa na koo hizo
ambapo serikali ilikataza eneo hilo
lisitumike kwa shughuli za kilimo ili kuepusha migogoro ya mara kwa mara.
Kamanda amesema kuwa baada ya Polisi kufika eneo hilo
hali ya utulivu imerejea katika vijiji
vya korotambe kubiterere ambapo kipindi
cha miaka mitatu iliyopita kumekuwepo na mapigano ya mara kwa mara baina ya koo
mbili za wanchari wakira na waryachoka
kulikuwa kunapelekea watu kupotea
maisha kuchomewa nyumba Maghala ya chakula na chanzo kikubwa ni ardhi na wizi
wa Ng’ombe.
Comments
Post a Comment