MWANAUME MMOJA WILAYANI BUNDA AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA YA KUMTOROSHA MWANAFUNZI NA KUMZALISHA WATOTO WAWILI


MWANAUME mmoja anayetuhumiwa kutorosha mwanafunzi wa shule ya sekondari Kibara, iliyoko wilayani Bunda, mkoani Mara, kwa zaidi ya miaka mitatu, amekamatwa na kufikishwa katika mahakama ya wilaya ya Bunda, akiwa tayari amekwishamzalisha mwanafunzi huyo watoto wawili.

Mwanaume huyo Joel Joseph, amekamtwa juzi mjini Musoma, wakati akiwa ndani ya daradara baada ya kuwekea mtego na mzazi wa mwanafunzi huyo, mwalimu Eward Masatu.
Mtuhumiwa huyo anadaiwa kumtorosha mwanafunzi huyo aitwaye Nyafwele Edward au Edina Edward, aliyekuwa anasoma kidato cha tatu katika shule ya sekondari Kibara, na kuishi naye kama mke wake, tangu mwaka 2009.

Imeelezwa kuwa Novemba 18, 2009 mtuhumiwa pamoja na mwanafunzi huyo, wote walikamatwa na kufikishwa katika kituo kidogo cha polisi Kibara, lakini kesho yake wakatoroka katika mazingira ya kutatanisha na kwamba walikuwa wakiishi katika miji mbalimbali ikiwemo Musoma, Tarime, Mwanza na Kahama.

Mwalimu Masatu amesema kuwa kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo kumetokana na mtego wake aliouweka, baada ya mtoto wake kupata ujauzito wa pili na kurejea nyumbani kwao kwa ajili ya kujifungua huku akimuomba mzazi wake amsamee.

Amesema kuwa baada ya binti yake kumuomba radhi alimkubalia na baada ya kujifungua walianza kumfuatilia mwanaume huyo, ambapo juzi alikamatwa na jana akafikisha katika mahakama ya wilaya ya Bunda, mbele ya hakimu wa mahakama hiyo, Safina Simfukwe.
Mwendesha mashitaka wa mahakama hiyo, Bw. Masuod Mohamed, baada ya kumsomea mashitaka yake, mtuhumiwa huyo alikana na amepewa dhamana baada ya kudhaminiwa na watu wawili, ambapo kesi yake itatajwa tena novemba 16, mwaka huu.
Chanzo:Ahmed makongo, Bunda

Comments

Popular posts from this blog

KATI YA KUKU NA YAI KIPI KILITANGULIA?

NGUO ZA NDANI ZINAZOBANA KWA WANAUME ZINAATHIRI UWEZO WA MBEGU ZA KIUME KUWEZA KUTUNGA MIMBA

TOZI GAMBA AFUNIKA SHOW YAKE NA THE TRACK MASTERS DJS BWALO LA POLISI MWISENGE SIKU YA CHRISTMAS