JINSI YA KUPATA MTAJI NA NAMNA YA KUTUMIA MTAJI KATIKA BIASHARA

 

JINSI YA KUPATA MTAJI NA NAMNA YA KUTUMIA MTAJI KATIKA BIASHARA

MTAJI

Mtaji ni kitu chochote ambacho unaweza kutumia katika kuzalisha kitu kingine kwa lengo la kupata faida.Biashara oyote iwayo lazima ianze na mtaji. Kuna aina tano za mitaji kama ifuatavyo:-
1. Mtaji wa fedha( financial capital)
2. binadamu mwenyewe( human capital) vitu kama ujuzi, elimu na kufanya kazi kwa bidii.
3. Jamii ( social network capital) ushirikiano na watu wengine katika biashara
4. utamaduni halisi wa mjasiliamali- utamaduni wa kufanya kazi kwa bidii,historia ya familia
5. fani au utaalamu  katika jambo flani

JINSI YA KUPATA MTAJI.

hapa tunaangalia vyanzo vya mtaji kwa mjasiliamali. Wajasiliamali wengi wanapata changamoto kubwa katika kupata mitaji ya kuanzishia biashara. nivigumu kuanzisha biashara bila kuwa na mtaji wa kutosha,hivyo basi mtaji ni muhimu sana lakini mtaji pekeyake hautoshi kuanzisha biashara ni lazima uwe na elimu ya ujasiliamali ili uweze kufanikiwa katika biashara. kuna njia mbalimbali za kupata mtaji na njia hizo zimegawanyika katika mafungu mawili ambayo ni chanzo cha ndani na chanzo cha nje.

Chanzo cha ndani ( internal sources of capital)

1. Mtaji   toka kwa mjasiliamali mwenyewe. huu ni mtaji ambao mjasiliamali anakuwanao kabla hajaanza biashara. huu ni mtaji bora sana kwani humilikiwa na mjasiliamali mwenyewe na hatakiwi kurudisha rejesho hata baada ya kupata faida.
2. Mtaji ambao unapatikana wakati biashara injiendesha. faida inayopatikana katika biashara inaweza kutumika kama mtaji. njia hii ndio huchangia kukua kwa biashara.
3. hisa. baadhi yawajasiliamali wanaweza kuamua kuwekeza katika hisa za makampuni. uwekezaji katika hisa husaidia kupata mtaji pale ambapo kampuni litagawa faida kwa wanachama waliowekeza katika hisa. pia mjasiliamali anaweza kupata mtaji kwa kuuza hisa kwa mtu mwingine au muwekezaji wa nje.

chanzo cha nje ( external sources of capital)

hapa tunaangalia mtajia ambao mjasiliamali anaweza kuupata toka nje ya yeye mwenyewe. baadhi ya vyanzo    hivyo ni kama ifuatavyo.
1. mkopo toka benki
huu ni mkopo ambao ulipaji wake ni wa muda mrefu.viwango vyariba si vikubwa sana ambavyo mjasiliamali anaweza kumudu kulipa endapo biashara itafanikiwa. mikopo ya benki inahitaji dhamana ya vitu visivyo hamishika mfano nyumba, shamba nk. 
 
Chanzo:gjob.blogspot.com

Comments

Popular posts from this blog

KATI YA KUKU NA YAI KIPI KILITANGULIA?

NGUO ZA NDANI ZINAZOBANA KWA WANAUME ZINAATHIRI UWEZO WA MBEGU ZA KIUME KUWEZA KUTUNGA MIMBA

MADHARA YA KUTUMIA DAWA ZA SILKONI KUONGEZA MAKALIO KWA WANAWAKE