Ashindwa Kutongoza Mademu, Ajaribu Kumbaka Bibi Yake

Kijana mwenye umri wa miaka 20 wa nchini Marekani ambaye alikuwa akilalamika kuwa anashindwa kumwaga sera za kuwavutia mabinti, aliamua kumpiga nyundo ya kichwa bibi yake ili apunguze haja zake za kimapenzi.
Samuel Dye alimfuata bibi yake na kuanza kulalamika kuwa ameshindwa kabisa kutongoza wanawake hivyo ameshindwa kupata mpenzi.

Taarifa za polisi zinasema kuwa Samuel baada ya kutoa malalamiko yake kwa bibi yake mzaa baba yake, alimuambia kuwa lakini ukame wake wa mapenzi angeumaliza siku hiyo kwake yeye.

Samule alishusha nguzo zake na kumuonyesha bibi yake nyeti zake kabla ya kumpiga nyundo ya kichwa ili aweze kutimiza azma yake ya kumaliza ukame wa mapenzi.

Taarifa zaidi zilisema kuwa Samuel alizuiliwa na baba yake asimbake bibi yake baada ya baba yake kusikia kelele za mama yake mwenye umri wa miaka 61 akiomba msaada baada ya kupigwa nyundo ya kichwa.

Baba mtu alimkuta mwanae akiwa ameshusha suruali yake akiendelea kumpiga na nyundo bibi yake.

Samuel alizidiwa nguvu na baba yake na alifungiwa kwenye chumba huku polisi wakiitwa waje kumchukua.

"Alikuja nyumbani saa 10 usiku akiwa na nyundo mkononi na kuanza kulalamika ameshindwa kupata mpenzi na leo ndio angemaliza tatizo hilo", alisema bibi yake Samuel na kuongeza "Nilimuomba asifanye chochote na tukae pamoja tusali tumuombe mungu".

Samuel ametiwa mbaroni na amefunguliwa mashtaka ya kujaribu kuua na kujaribu kubaka.Tembelea www.Nifahamishe.com
   

Comments

Popular posts from this blog

KATI YA KUKU NA YAI KIPI KILITANGULIA?

NGUO ZA NDANI ZINAZOBANA KWA WANAUME ZINAATHIRI UWEZO WA MBEGU ZA KIUME KUWEZA KUTUNGA MIMBA

TOZI GAMBA AFUNIKA SHOW YAKE NA THE TRACK MASTERS DJS BWALO LA POLISI MWISENGE SIKU YA CHRISTMAS