Posts

Showing posts from 2014

Timu ya wachezaji watumishi wa manispaa ya musoma ipo njia panda kwenda kushiriki katika mashindano ya shirikisho la michezo serikali za mitaa Tanzania Shimisemta

Timu ya wachezaji   watumishi wa manispaa ya musoma huenda ikashindwa kushiriki katika mashindano ya shirikisho la michezo serikali za mitaa Tanzania Shimisemta, baada ya wachezaji wa timu hiyo kudai kuwa hajapewa fedha toka katika ofisi ya mkurugenzi kwa ajili ya kwenda kushiriki katika mashindano hayo yanayotarajiwa kufanyika huko morogoro. Wakiongea kwa sharti la kutotajwa majina yao baadhi ya watumishi hao wamesema japokuwa wamekuwa wakitenga muda wao kufanya mazoezi kwa ajili ya kujiandaa na mashindano hayo lakini wanashindwa kufanya mazoezi kwa uhakika kutokana na mkurugenzi wa manispaa ya musoma mpaka   kutowathibitishia kwenda kushiriki   katika mashindano huku zikiwa zimebaki siku nne mashindano hayo kuanza. Wachezaji hao wamedai kuwa wanashindwa kuelewa toka mwaka 2000 timu ya watumishi wa manispaa ya musoma haijashiriki katika mashindano hayo kwa kisingizio cha ufinyu wa bajeti lakini   timu za manispaa ya Musoma vijijini, Bunda, Serengeti pamoja na Tarime zim

WANAFUNZI WA MARA SEKONDARI WAANDAMANA WAKIDAI MATIBABU BORA NA CHAKULA BORA

Image
WANAFUNZI WA MARA SEKONDARI WAKIWA KATIKA MAANDAMANO                           Wanafunzi wa shule ya  Sekondari  ya Mara iliyopo  Manispaa ya Musoma mkoani Mara leo wameandamana kuelekea ofisi za mkoa   kile wanachodai kuwa katika shule hiyo hakuna utaratibu  bora wa matibabu na kubadilishiwa   ratiba ya Chakula. Wakiongea mbele ya Afisa Elimu Mkoa wa Mara Bw Hamis Lisu katika viwanja vya Posta Manispaa ya Musoma, Baadhi ya wanafunzi hao wamesema kuwa kubadilika kwa ratiba ya chakula na kutokuwepo kwa huduma bora za matibabu ndio hali iliyopelekea wao kuandamana ili kufikisha kilio chao katika ngazi ya mkoa. Wamesema kuwa walipokuwa kidato cha tano ratiba ya kula wali,nyama pamoja na mboga za Majani ilikuwa ni mara mbili kwa wiki lakini tangu January Mwaka huu walielezwa kubadilika kwa ratiba ya chakula kutokana na kugoma kwa mzabuni na hivyo kula wali na nyama mara moja kw wiki  huku mboga za majani hazipatikani kabisa kama wanavyobainisha Alex Mirumbe pamoja na E
Emmanuel Chibasa-Mara Watu wenye ulemavu mkoani Mara wamekutana na uongozi wa mkoa wakiwemo madiwani, wakuu wa idara, pamoja na maafisa maendeleo ya jamii, lengo ikiwa ni kuitambulisha   miongozo ya kitaifa na kimataifa inayoelezea mahitaji na hali halisi ya watu wenye ulemavu ili waweze waweze kuingizwa kwenye mipango kazi pamoja na Bajeti za Halmashauri. Akiongea katika kikao hicho Abdala Omari ambaye ni mmoja ya wajumbe ya wajumbe wa chama cha walemavu Tanzania SHIVYAWATA ,amesema wameamua kutambulisha miongozo hiyo ili kupunguza changamoto zinazowakabili watu wenye ulemavu kwa kuingizwa kwenye bajeti za Halmashauri hapa nchini ili kuondokana na utegemezi katika jamii. INSERT: Abdala Omary-Mjumbe Shivyawata Batista Mgumba ni mwezeshaji kutoka chama cha wasioona Tanzania amesema imefika wakati maswala ya watu wenye ulemavu Tanzania inatakiwa yaingizwe kwenye bajeti za halmashauri wakati wa kupanga mipango pamoja na kupanga bajeti ili waweze kupata huduma sawa k
25 Oct 2014 TIMU ya Polisi Mara imeondoka kuelekea mkoani Shinyanga kucheza mchezo wake wanne dhidi ya timu ya Mwadui huku ikitoa tambo ya kufanya mizuri kwenye mchezo huo kutokana na uelewano wa wachezaji. Akizungumza kabla ya kuondoka kwa timu hiyo yenye maskani yake mjini musoma Afisa Habari wa timu hiyo Musa Keita amesema timu hiyo inaenda kucheza mchezo wa ugenini ikiwa na pointi 7 ikiwa ni ushindi wa michezo miwili na sare moja katika michezo iliyotangulia imewaweka wachezaji katika ari nzuri ya kufanya vizuri kwenye mchezo huo. Amesema kwa sasa kikosi cha timu hiyo kipo kwenye maelewano mazuri uwanjani ndio sababu inayowapa Imani ya kufanya vizuri kwenye mchezo wa dhidi ya Mwadui hapo kesho. Keita alisema wanaondoka kwenda kwenye michezo ya ugenini wakiamini kufanya vizuri kuanzia mchezo huo dhidi ya Mwadui kabla ya kuzifuata timu za JKT Kanembwa na polisi ya Tabora na baadae kurudi nyumbani kwenye michezo mingine. Akizungumzia michezo mitatu iliyotangul