Emmanuel Chibasa-Mara

Watu wenye ulemavu mkoani Mara wamekutana na uongozi wa mkoa wakiwemo madiwani, wakuu wa idara, pamoja na maafisa maendeleo ya jamii, lengo ikiwa ni kuitambulisha  miongozo ya kitaifa na kimataifa inayoelezea mahitaji na hali halisi ya watu wenye ulemavu ili waweze waweze kuingizwa kwenye mipango kazi pamoja na Bajeti za Halmashauri.

Akiongea katika kikao hicho Abdala Omari ambaye ni mmoja ya wajumbe ya wajumbe wa chama cha walemavu Tanzania SHIVYAWATA ,amesema wameamua kutambulisha miongozo hiyo ili kupunguza changamoto zinazowakabili watu wenye ulemavu kwa kuingizwa kwenye bajeti za Halmashauri hapa nchini ili kuondokana na utegemezi katika jamii.

INSERT: Abdala Omary-Mjumbe Shivyawata

Batista Mgumba ni mwezeshaji kutoka chama cha wasioona Tanzania amesema imefika wakati maswala ya watu wenye ulemavu Tanzania inatakiwa yaingizwe kwenye bajeti za halmashauri wakati wa kupanga mipango pamoja na kupanga bajeti ili waweze kupata huduma sawa kama walivyo watu wengine.

INSERT: Batista Mgumba-Mwezeshaji Chama cha Wasioona Tanzania

Kwa upande wake mwanaharakati wa kutetea haki za watu wenye ulemavu Elieza Mdakilwa amesema kutokana na watu kutokua na mwamko wa kutetea haki za watu wenye ulemavu hapa mchini ametoa wito kwa taasisi zinazojihusisha na maswala ya watu wenye ulemavu zinatakiwa kuendelea kutetea haki za watu wenye ulemavu kunzia ngazi ya serikali za mitaaa mpaka serikali kuu.

INSERT: Elieza Mdakilwa-Mwanaharakati

Takwimu zinaonyesha kuwa  mkoa wa Mara unaongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya watu wenye ulemavu hapa nchini kwa kuwa  asilimia 13.
Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

KATI YA KUKU NA YAI KIPI KILITANGULIA?

NGUO ZA NDANI ZINAZOBANA KWA WANAUME ZINAATHIRI UWEZO WA MBEGU ZA KIUME KUWEZA KUTUNGA MIMBA

TOZI GAMBA AFUNIKA SHOW YAKE NA THE TRACK MASTERS DJS BWALO LA POLISI MWISENGE SIKU YA CHRISTMAS